Mbosso - Darasa La Saba (Lyrics)




INTRO

Mwishoni darasa la saba

Mimi na yeye ndio tulijuana

Sababu ya kukosa Ada

Mi kidato ikashindika


VERSE 1

Ndoto za udakitari

Kwisha habari

Zikapeperuka

Na yeye sekondari

Akaamishwa mbali

Mkoani Arusha


PRE-CHORUS

Hisia na balehe zilikutana kati

Mambo ya kupenda

Ujana maji ya moto

Eh moyo ngoja basi

Nikaja kusikia

Yuko gongo la mboto

Mara chuo Mtwara, Masasi

Nyie Wahenga waongo

Mambo ya dunia ndogo

Mbona sijui sasa yupo wapi


CHORUS

Namtafutaaa...


Bado namtafuta, mchumba wangu wa darasa la saba

Ajue sikuchezea fursa, ni wazazi walikosa ada

Bado namtafuta, mchumba wangu wa darasa la saba

Ajue sikuchezea fursa, ni wazazi walikosa ada


POST-CHORUS / REFRAIN

Tere liye, tere sanam

Tere liye, tere sanam

Tere liye, tere sanam

Tere liye, tere sanam


VERSE 2

Mara ya mwisho kumuona

Ni siku ya mahafali

Niliandika ujumbe ila hakuusoma

nyuma ya daftari

Suluhisho Mi kupona nijue angali

mzima yupo salama niache kusonona

Moyo upate afadhali


BRIDGE

Nikimuona nitamusimulia

Yote niliyoyapitia

Ajue yeye ndio chanzo cha Mimi kuishi Duniani


Nilivyommisi nitamkumbatia

Uenda naye kanimisi pia

Ni mawazo yanayonizunguka kichwani


VERSE 3 (REPEAT)

Ndoto za udakitari

Kwisha habari

Zikapeperuka

Na yeye sekondari

Akaamishwa mbali

Mkoani Arusha


PRE-CHORUS (REPEAT)

Hisia na balehe zilikutana kati

Mambo ya kupenda

Ujana maji ya moto

Eh moyo ngoja basi

Nikaja kusikia

Yuko gongo la mboto

Mara chuo Mtwara, Masasi

Nyie Wahenga waongo

Kwamba dunia ndogo

Mbona sijui sasa yupo wapi


CHORUS (FINAL)

Namtafutaaa...


Bado namtafuta, mchumba wangu wa darasa la saba

Ajue sikuchezea fursa, ni wazazi walikosa ada

Bado namtafuta, mchumba wangu wa darasa la saba

Ajue sikuchezea fursa, ni wazazi walikosa ada



OUTRO

Tere liye, tere sanam

Tere liye, tere sanam

Tere liye, tere sanam

Tere liye, tere sanam

Post a Comment

Drop your comment here

Previous Post Next Post